Wadau wa facebook

Maelezo

Kwa matukio na matangazo wasiliana nasi Simu no' {301}728-3977. Email:swahilivilla@gmail.com

Wednesday, May 22, 2013

Vita mpya ya CCM, CHADEMA bungeni

MWENENDO wa Bunge la Bajeti linaloendelea mjini hapa, umebaini kuwa vita ya maneno, fitna kati ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), sasa imehamia bungeni, Tanzania Daima Jumatano limebaini.

Moto wa vita hiyo kati ya vyama hivyo hasimu, umekolezwa zaidi baada ya Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete kufanya mkutano wa kimkakati na wabunge wa chama chake mjini hapa.

Duru za siasa kutoka ndani ya kikao hicho cha wabunge na rais, zilieleza kuwa Rais Kikwete aliwataka wabunge hao wa CCM wajipange kukabiliana na hoja za CHADEMA ambazo katika siku za hivi karibuni zimeonekana kulitikisa Bunge kiasi cha kiti cha spika kuamua kutumia kanuni kandamizi kuzizima.

Wabunge wa CCM bila kujali uzito wa hoja, wameamua kukabiliana na hoja zozote za wabunge wa CHADEMA hata kama zina maslahi kwa taifa.

Tayari CHADEMA kimeeleza kubaini mbinu hizo, kikidai kuwa hata kitendo cha Spika Anne Makinda kukatisha hotuba ya msemaji wao katika Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Joseph Mbilinyi ilikuwa sehemu ya utekelezaji wa mkakati huo.

Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CHADEMA, John Mnyika alisema kuwa hatua hiyo ndiyo iliwafanya wasikubali kubadili hotuba yao hiyo kuanzia ukurasa wa kwanza hadi wa 14 kama ilivyotakiwa na spika kwani ni kinyume na kanuni ya 63 (2).

Tuesday, May 21, 2013

President Obama Speaks on the Tornadoes and Severe Weather in Oklahoma

President Obama delivers a statement about the ongoing response efforts following the devastating tornadoes in Oklahoma.

Edward Hoseah: Tunaweza kukomesha rushwa Tanzania

Mhojiano yalifanywa na Deodatus Balile, Dar es Salaam

Edward Hoseah, mpambanaji wa juu kabisa wa Tanzania dhidi ya rushwa katika viwango vyote vya serikali, anasema nchi inaweza kujinasua na athari za ubovu wa rushwa na kuwa moja ya nchi zenye rushwa ndogo kabisa duniani.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Edward Hoseah akizungumza na mashirika ya asasi za kijamii juu ya mafanikio ya taasisi hiyo hadi sasa katika Hoteli ya Mövenpick jijini Dar es Salaam mwezi Machi 2012. [Na Deodatus Balile/Sabahi]

Hoseah anaongoza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) nchini na pia ni mwenyekiti wa Bodi ya Umoja wa Afirika (AU) ya Kupambana na Rushwa.

Tangu alipochukua nafasi ya mkurugenzi mkuu wa TAKUKURU mwaka 2006, taasisi hiyo imesaidia sana kupunguza rushwa na kuimarisha nafasi ya Tanzania katika orodha ya rushwa duniani kote, Hosea anaiambia Sabahi katika mahojiano.

Lakini licha ya mafanikio hayo, Hosea anasema kuwa taasisi yake inahitaji na kupewa mamlaka zaidi ili kuwa ya mafanikio zaidi, ikiwa ni pamoja na nguvu za kushitaki.

Sabahi: Ziko wapi kazi kuu zilizokabidhiwa TAKUKURU?

Edward Hoseah: Wajibu wetu mkuu ni kuzuia rushwa nchini. Tunaishughulikia rushwa kutoka pande tatu. Kwanza ni kuzuia, ambako kunajumuisha usimamiaji wa kiwango [kikubwa] cha uhawilishaji fedha na kuchunguza mienendo ya kisasa [juu ya vipi watu wanabadilishana fedha].

Spika wa bunge aliahirisha bunge kwa dharura kujadili hotuba ya kambi ya upinzani.

Spika wa bunge Mh. Anne Makinda ameliahirisha bunge kwa dharura kupisha kamati ya kudumu ya kanuni za bunge kukutana kwa ajili ya kuijadili hotuba ya kambi rasmi ya upinzani iliyokuwa ikisomwa bungeni kwa madai ya kuwa na baadhi ya maneno ya uchochezi na baadae kutoa maamuzi ya kuondolewa kwa maneno yote yaliyoko katika ukurasa wa kwanza hadi 14 wa hotuba hiyo.

UN kuwa na wasiwasi wa kuzuka tena mapigano Nchini Congo

Umoja wa Mataifa umesema kuwa, una wasi wasi wa kuzuka tena machafuko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. 

Msemaji wa Umoja wa Mataifa ametangaza kuwa, vikosi vya kusimamia amani vya Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo vimeelezea wasi wasi wake wa kuanza tena mapigano baina ya vikosi vya serikali na waasi wa M23 jirani na mji wa Goma mashariki mwa nchi hiyo. 

Eduardo del Buey, Naibu Msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amewaambia waandishi wa habari kwamba, kumezuka mapigano katika maeneo ya Kibati na Rusayo yapata kilomita 12 kutoka katika mji wa Goma baina ya wapiganaji wa waasi wa M23 na vikosi vya serikali ya Kinshasa. 

Eduardo del Buey ameongeza kuwa, vikosi vya kusimamia amani vya Umoja wa Mataifa vilivyoko Congo DRC vimeripoti kwamba, pande mbili zilitumia silaha nzito katika mapigano hayo. 

Katika upande mwingine, Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imepanga kujenga bwawa litakalokuwa kubwa zaidi duniani itakapofika mwaka 2015. 

Taarifa zinasema kuwa, bwawa hilo lilikuwa lijengwe miaka kadhaa iliyopita, lakini ilishindikana kutokana na ukosefu wa fedha za kugharamia ujenzi huo.

Saudi Arabia detains 10 more in Iran-linked spy case

Spokesman for the Saudi Interior Ministry, Mansour al-Turki, said in April that initial investigation has revealed direct involvement of those arrested with Iranian intelligence. (File Photo: AFP)

Al Arabiya with Agencies -

Saudi authorities have detained 10 more suspects in an alleged Iranian spy ring it announced in March, an Interior Ministry spokesman said on Tuesday.

“Initial investigation carried out by the authorities led to the detention of 10 others for involvement in spying activities,” state television news channel al-Ekhbariya reported, citing the Interior Ministry.

The suspects include eight Saudis, a Lebanese and a Turk, it said.

On March 19, the Interior Ministry said authorities had arrested 16 Saudis, an Iranian and a Lebanese in four regions including the Eastern Province.

While Iran has denied any involvement in the alleged spy ring, spokesman for the Saudi Interior Ministry, Mansour al-Turki, said in April that initial investigation has revealed direct involvement of those arrested with Iranian intelligence.

Rais Kikwete kuzindua miradi ya ujenzi wa barabara ya Dodoma-Iringa.

Dr-Jakaya-Mrisho-Kikwete
RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHE. DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE KUZINDUA MIRADI YA UJENZI WA BARABARA YA DODOMA – IRINGA YENYE UREFU WA KM 260 (SEHEMU ZA DODOMA – FUFU ESCARPMENT, FUFU ESCARPMENT – MIGORI NA MIGORI – IRINGA) KWA KIWANGO CHA LAMI TAREHE 22 MEI, 2013

Wizara ya Ujenzi inapenda kutoa taarifa kwa Umma kwamba, tarehe 22 Mei, 2013 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete atakuwa mgeni Rasmi katika sherehe za uzinduzi wa miradi ya ujenzi wa barabara kama ifuatavyo:-

1) Tarehe 22 Mei, 2013 Asubuhi kuweka jiwe la msingi sehemu ya Dodoma – Fufu Escarpment (km 93.8) katika eneo la Dodoma Mjini.

2) Tarehe 22 Mei, 2013 Mchana kuweka jiwe la msingi sehemu ya Fufu Escarpment – Migori (km 70.9) na Migori – Iringa (km 95.3) katika Kijiji cha Migori Wilayani Iringa Vijijini.

Barabara ya Iringa – Dodoma ni sehemu ya barabara muhimu ijulikanayo kama “Great North Road” inayoanzia Capetown Afrika ya Kusini hadi Cairo, Misri kupitia Tanzania. Nchini Tanzania inaunganisha Miji ya Tunduma (mpakani na Zambia), Mbeya, Iringa, Dodoma, Arusha na Namanga (mpakani na Kenya).

Press Briefing

White House Press Briefings are conducted most weekdays from the James S. Brady Press Briefing Room in the West Wing.

Watu 91 wauwawa kwa kimbunga 20 wakiwa watoto wa shule nchini Marekani

Horror: Teachers carry children away from Briarwood Elementary school after a tornado destroyed the school in south Oklahoma City
Walimu waliojitolea kubeba mtoto katika shule BRIARWOOD Elementary baada ya kuathirika vibaya kwa kimbunga kilichoharibu shule ya kusini mwa Oklahoma City. (Photo.dailymail.co.uk)

Kimbunga kikubwa cha Tornado kimeukumba mji wa Oklahoma mapema leo Jumatatu na kubomoa vitalu vya nyumba, shule mbili na kuua takribani watu 91 ikiwa ni pamoja na watoto 20, viongozi wa mitaa wamearifu.

Rais Obama amesikitishwa na tukio hilo na kuliita janga kubwa ambapo Kikosi cha uokozi kimeendelea na jitihada za kutafuta manusura katika mabaki ya majengo.

Fear: A child calls to his father after being pulled from the rubble of the Tower Plaza Elementary School    Brave: A boy is pulled from beneath a collapsed wall at the Plaza Towers Elementary School following a tornado in Moore, Oklahoma
Waokuaji  wakiendelea kuogoa baadhi ya watotho waliokumbwa vibaya kwa kimbunga katika Shule Plaza Towers Elementary kufuatia kimbunga kilichoathiri vibaya huko Moore, Oklahoma. (Photo.dailymail.co.uk)


Ofisi ya mtabibu wa serikali imetoa taarifa ya karibuni kuhusu idadi ya waliopoteza maisha lakini idadi hiyo inaongezeka kwa kasi, wakati kikosi cha huduma ya dharura wamesafisha mabaki yote ya nyumba zilizobomolewa pamoja na shule katika kitongoji cha Moore mjini Oklahoma.

Watabiri wa hali ya hewa wamearifu kuhusu uwepo wa upepo mkali wa maili mbili, na helikopta ya habari za televisheni imenasa faneli zito likipita katika vitongoji kadhaa.

Gavana wa Oklahoma Mary Fallin ameviambia vyombo vya habari kuwa kimbunga hicho ni kikubwa zaidi kuwahi kutokea katika eneo hilo akiongeza kuwa majeruhi ni wengi na uharibifu mkubwa wa miundo mbinu umefanyika.

Naye mkuu wa polisi katika kitongoji cha Moore Jerry Sillings amewataka wakazi wa kuondoka katika eneo hilo wakati masuala kadhaa ya kiusalama yakifanyika.

Survivors: A child is pulled from the rubble of the Plaza Towers Elementary School in Moore, Oklahoma, and passed along to rescuers
Waathirika: Uendelezaji uwokoaji wa watoto katika Shule ya Plaza Towers Elementary huko Oklahoma (Photo.dailymail.co.uk)

Tanzania to host Smart Partnership dialogue forum next June

The Global Smart Partnership Dialogue in the country will send out a clear message to all the technologically advanced countries that, Tanzania has geared itself towards the dialogue on technology.

Minister for Foreign Affairs and International Co-operation, Hon Bernard Membe
Minister for Foreign Affairs and International Co-operation, Hon Bernard Membe

Speaking in Dar es Salaam Minister of Foreign Affairs and International Cooperation Mr Bernard Membe said that the meeting is expected to bring changes in the country in socio-economic status throughout the world.

Mr Membe noted that Smart Partnership meeting is a forum for developing countries which will be deliberate on science and technology for economic development of the countries. Mr Membe said the meeting will be held in Dar es Salaam between June 28th and 1st July this year.

“Technology is a crucial catalyst for developing nations’ development in this world,” he said. He noted that Tanzania will be the hosts of Smart Partnership scheduled to be held in Dar es Salaam and to be attended by 500 delegates including five presidents from East African states.

The Global Smart Partnership Dialogue which will be held in Tanzania, amongst other things, would get feedback from the last dialogue that was held in Putrajaya, Malaysia in June last year.

Other African countries that have hosted the Smart Partnership Dialogues include Botswana, Namibia, Zambia, Zimbabwe, Mozambique, Swaziland, Lesotho and Uganda. Other countries include Barbados, and Malaysia.

Maalim Seif amevitaka vyombo vya ulinzi nchini kusimamia vyema majukumu yake

Na Hassan Hamad, OMKR

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, amevitaka vyombo vya ulinzi nchini kusimamia vyema majukumu yake ili kuhakikisha kuwa bahari na mipaka ya nchi inakuwa salama.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akizungumza na Mkuu wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar, Brigedia Jenerali S S Othman, alipofika ofisini kwake Migombani.

Amesema Zanzibar ikiwa nchi ya visiwa, inakabiliwa na changamoto moto nyingi za kiulinzi na usalama kuhakikisha kuwa magaidi hawaingii nchini, sambamba na kukabiliana na vitendo vya uharamia na usafirishaji wa dawa za kulevya.

Maalim Seif ameeleza hayo ofisini kwake Migombani alipokuwa na mazungumzo na Mkuu wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar, Brigedia Jenerali S S Othman.

Amesema katika siku za hivi karibuni kumekuwa ni tishio la vitendo vya kigaidi katika Pembe ya Afrika, jambo ambalo linapaswa kuzingatiwa ili vitendo hivyo visije kuiathiri Zanzibar.

“Suala la ulinzi halina mbadala, kitu cha msingi ni kwa vyombo vya ulinzi na dola kushirikiana kuhakikisha kuwa nchi iko salama kwa maslahi ya wananchi na taifa kwa ujumla”,alisisitiza Maalim Seif.

Kuhusu vitendo vya uharamia vinavyofanywa katika bahari ya hindi, Maalim Seif amesema vinaathiri shughuli za kibiashara na uchumi na vinastahiki kupigwa vita kwa nguvu zote.

Kwa upande wake, Mkuu wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar, Brigedia Jenerali S S Othman, amesema suala la ulinzi ndio jukumu la msingi kwa vyombo vya ulinzi, na kuahidi kushirikiana na vyombo vya dola na wananchi katika kutekeleza jukumu hilo kwa ufanisi zaidi.

President Obama's Bilateral Meeting with President Thein Sein of Myanmar

President Obama and President Thein Sein of Myanmar speak to the press after a bilateral meeting in the Oval Office.

Polisi wakamatwa na bangi gunia 18

WAISAFIRISHA KWA GARI LA MKUU WA FFU

Na Charles Ndagulla, Moshi

SIKU chache baada ya Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kuwakamata askari 16 wakituhumiwa kujihusisha na biashara ya magendo, askari wengine wawili wa jeshi hilo wamekamatwa mkoani Kilimanjaro wakiwa na shehena kubwa ya bangi wakiisafrisha kwenda nchini Kenya.

Askari hao walikamatwa Mei 19 mwaka huu saa nne usiku eneo la Kilemapofu, Wilaya ya Moshi Vijijini wakiwa na magunia 18 ya bangi ambayo walikuwa wameyapakia kwenye gari la Mkuu wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) mkoani Arusha aina ya Toyota Land Cruiser lenye namba PT 2025.

Akithibitisha kukamatwa kwa askari hao, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz alisema askari hao walikuwa wakipeleka bangi hiyo Wilaya ya Rombo kwa mfanyabiashra mmoja ambaye hakutaka kumtaja jina lake.

Kamanda Boaz aliwataja askari waliokamatwa na wanashikiliwa kwenye kituo kikuu cha polisi katika mji mdogo wa Himo kuwa ni F.1734 Koplo Edward (dereva) wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) mkoani Arusha na G.2434 Konstebo George wa kituo cha polisi Ngarenanyuki Wilaya ya Arumeru.